Mti wa Ujuzi - 3. Maarifa (Ujuzi), Mema na Mabaya (Seh. 2)
Download and listen anywhere
Download your favorite episodes and enjoy them, wherever you are! Sign up or log in now to access offline listening.
Mti wa Ujuzi - 3. Maarifa (Ujuzi), Mema na Mabaya (Seh. 2)
This is an automatically generated transcript. Please note that complete accuracy is not guaranteed.
Description
Nyoka hufahamika kama shetani na inaandikwa hivyo. Lakini wanadamu wa tabia za mwili hawafahamu upande wa pili wa kile kinachofahamika kama nyoka! Neno la Kiebrania Tov טוב lina maana na...
show more• Aleph א ni namba 1
• Daleth ד ni namba 4
• Mem ם ni namba 40
Numerologia huzingatia namba 0 hadi 9 maana namba yoyote juu ya 9 ni marudio kati ya 0 hadi 9 yenyewe. Hivyo tunajumlisha kwa namna hii:
1+4+4+0=9
Hii tunaona ndiyo sababu mwanadamu hukaa miezi 9 tumboni mwa mamaye. Turejee ya kwamba namba 9 ni ile herufi Tet ambayo ina maana ya nyoka. Vile vile nyoka hakuondolewa ndani ya bustani ya Eden mara baada ya anguko kwa Adam na Eva ila tunaona wawili hawa ndiyo waliondolewa.
Kitendo cha kuondolewa Eden ni kile tunachokiita mwanadamu kuzaliwa katika mwili wa damu na nyama yaani huu mwili wa uharibifu. Na ndiyo maana kwa asili kila mwanadamu ni mwana wa Adam kwa maana ya 9 yaani herufi Tet ט katika namna ya anguko. Hii ni sababu wengi hawaelewi ni kwanini rabbi Yesu alisema:
Enyi nyoka, wana wa majoka, mtaikimbiaje hukumu ya jehanum?
Mathayo 23:33
Wana wa majoka ni wana wa herufu Tet ט katika anguko yaani nje ya bustani ya Eden hivyo tunalithibitidha hilo katika maarifa kwa kile kinachotokea yaani nafsi kuja katika mwili katika ukamilifu wa 9 yaani kwa kupitia miezi 9. Tukiwa katika mwili rabbi Yesu akasema:
..basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.
Mathayo 10:16b
Kuwa na busara kama nyoka huu ni upande mwingine tofauti wa kile kinachofahamika kama nyoka. Huyu ni nyoka wa Musa. Huyu ni yule nyoka wa Brasi (na siyo shaba kama inafvitafsiriwa) ambaye Musa alimwinua kwa ajili ya uponyaji wa wana wa Israeli. Mambo haya hunenwa kwa maarifa na si kimtizamo kusoma literally kama simulizi za kawaida.
Brasi (brass) ni muunganiko wa Zinki (zinc) na Shaba (copper) ambapo Zinki inawakilisha Adam na Shaba inawakilisha Eva. Matokeo ya muunganiko huko ndiyo kuinuliwa kwa nyoka ambapo katika neno Tov טוב lenya maana ya "mema", herufi ya mwisho ni Beth ב yenye maana ya hekalu/hema ambayo ina maanisha miili yetu na ndiyo maana miili yetu ni bustani ambapo herufi Vav ו ni mti (wa uzima) ambayo nyoka wa Brasi (Zinki+Shaba) yaani herufi Tet ט hutundikwa kwa ajili ya ya uzima.
Nyoka anapomshinda mwanadamu kwa jaribu huitwa shetani wakati nyoka anayeshindwa, kwa washindi huwa ni busara. Ndiyo maana ya kile asemacho rabi Yesu "..iweni na busara kama nyoka". Kadhalika hiki ndicho kile rabbi Yesu akimwambia Nikodemo:
Na kama vile Musa alivyomwinua yule nyoka jangwani, vivyo hivyo Mwana wa Adamu hana budi kuinuliwa;
Yohana 3:14
Mambo haya hupaswa kufanyika ndani yetu.
Kwa mengine zaidi, karibu tujifunze pamoja.
Unaweza wasiliana nasi kwa barua pepe:
tanzaniagnosishelpers@gmail.com
Information
Author | Tanzania Gnosis |
Organization | TanzaniaGnosis |
Website | - |
Tags |
-
|
Copyright 2024 - Spreaker Inc. an iHeartMedia Company